Thursday 10 January 2008

TAKEU style ipo wapi?

Jamani Mr. Nice mbona kimya sana ingawa unasema kuwa bado hujatetereka lakini kimya hiki kinaashiria nini?

Bongo Star Search iko juu!!!

Nani utampatia kijiti cha Bongo Star Search, Fikiri kwa makini.
Mnatakiwa kweli kuitwa majaji halisi. Salama upo makini! Big up sis!




Baadhi ya vituko vyao vya mwaka mzima 2007

Mpoki na Wakuvanga.
Masanja mkandamizaji na Joti mtoto wa mjini.

Tuanakumiss sana baba!!!

Mwalimu Nyerere(katikati),mama yake mzazi(kushoto) na mkewe Maria(kulia).Picha hii ilipigwa Novemba 10,1985 Butiama baada ya Nyerere kustaafu.

He was a simple man.
Shukran ya picha kutoka bongocelebrity.com

Mchezo huu ulithaminiwa sana enzi hizo. Hebu tuvienzi vitu hivi.

Mwinyi (wa pili kutoka kushoto) akishuhudia mchezo wa bao kati ya hayati Mwalimu Nyerere (wa pili kutoka kulia) na mzee mmoja wa Butiama(jina halijulikani).Wengine wanaoshuhudia ni Mama Maria Nyerere(kulia) na kaka yake Nyerere,Chief Burito(wa tatu kutoka kulia).Picha ilipigwa Butiama.

Fanya kazi mama.

Majadiliano na wa nyumbani muhimu sana kuapta nasaha za hapa na pale. Asha Rose Migiro akiwa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania. Mhe. Jakaya Kikwete.
Mheshimiwa Asha Rose Migiro akitoa hotuba.

Kanumba The Great! Serikali thaminini kazi za wasanii!

Kanumba akiwa na Wema Sepetu.





Kanumba katika pozi ni baadhi ya usanii wake.


Ajira kwa wakazi waishio jirani na Chuo

Wakinadada wakifua nguo za baadhi ya wanafunzi wa chuo kikuu cha Tumaini Iringa.

BBC enzi hizo!!

David Wakati mmoja wa watangazaji wa kwanza ambaye baadaye alirejea nyumbani Tanzania na kuwa mkuu wa redio ya taifa- RTD.
Mtangazaji Hassan Mazoa wa Idhaa ya Kiswahili ya BBC akijiandaa kwa kipindi cha muziki enzi hizo.

Zeyana Seif mmoja wa watangazaji wa kwanza wa kike akiwa na wenzake mwaka 1959.


Huyu ndiye hayati Oscar Kambona, mtangazaji aliyerusha matangazo ya kwanza ya Idhaa ya Kiswahili ya BBC tarehe 27 mwezi Juni mwaka 1957. Alifariki Uingereza akiwa na umri wa miaka 68.

Wametoka mbali!!


Mwaka 1955 jengo la Bush House, makao ya BBC World Service, lilikuwa ni eneo lenye shughuli nyingi sana kama inavyoonekana kwenye picha hii, Idhaa ya Kiswahili ilikuwa hapa.

Wednesday 9 January 2008

Tuesday 8 January 2008

Pole sana!!!


Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania akimfariji mhariri wa gazeti la Mwanahalisi ndugu Saed Kubenea alimwagiwa Tindikali machoni na watu wasiojulikana alielazwa katika hospitali ya Muhimbili Dar.